Mfahamu Sitti bint Saad mwanamke wa kwanza kuimba taarab hapa nchini

Sitti bin Saad
SITI Bint Saad ni mwimbaji mkongwe nchi aliyetokea kwenye familia dunia ambaye alibarikiwa kipaji cha pekee cha uimbaji.
Kipaji cha muimbaji huyo kilimsaidia sana tangu siku za awali za maisha yake kwani alitumia uimbaji wake kuuza vyungu vya mama yake alivyokuwa akimsaidia kuvitembeza.
Siti alijaliwa kuwa na sauti iliyoweza kupaa na kusafiri kwa umbali wa maili nyingi na hii ndio ilikuwa ishara ya watu kujua kwamba vyungu vyao vinapita.
Nguli huyo alifananishwa kuwa na mapafu yenye nguvu kama simba kutokana na alivyoweza kupaza sauti yake mbali bila kuachia pumzi.
Historia inaonyesha kwamba Siti alizaliwa katika kijiji cha Fumba, Zanzibari mwaka 1880 na baada ya kuzaliwa alipewa jina la 'Mtumwa' kwasababu alizaliwa katika kipindi cha utumwa wa Kiarabu. Jina la Siti alipewa na mkabaila mmoja wa kiarabu.
Baba yake Mzee Saadi alikuwa ni Mnyamwezi kutoka Tabora na mama yake alikuwa ni Mzigua toka Tanga, lakini wote wawili walizaliwa Zanzibari.
Hali ya maisha ya familia yao ilikuwa ni duni sana na walijishughulisha zaidi katika shughuli za kilimo na ufinyanzi kazi ambazo Siti alijifunza na kuzimudu vizuri.
Kama waswahili wasemavyo 'kuzaliwa masikini si kufa masikini' Siti kipaji cha uimbaji alichobarikiwa muimbaji huyo kilimsaidia siku za awali za maisha yake na alitumia kipaji hicho kuuza vyungu vya mama yake.
Kutokana na wakati huo elimu kwa watoto wa kike kutotiliwa mkazo, Siti hakuwahi kwenda shule wala kuhudhuria mafunzo ya kusoma Kurani.
Mnamo mwaka 1911 alihamia mjini ili kubooresha maisha yake.Ujio wake wa kuishi mjini ulikuwa wa neema kwani ulimkutanisha na muimbaji wa kundi la muziki wa taarabu la "Nadi Ikhwani Safaa" Muhsin Ali.
Katika kipindi hicho, kundi la Nadi Ikhwani Safaa lilikuwa kundi pekee la muziki wa taarabu lililoanzishwa na Sultani mpenda starehe na anasa Seyyid Barghash Said.
Kundi hilo lilikuwa la wanaume peke yake , wanawake hawakuruhusiwa kujiunga na vikundi vya muziki kwani ilikuwa ikichukuliwa kama ni uhuni.
Hata hivyo Muhsin alikiona kipaji cha pekee cha Siti na hivyo akajitolea kumfundisha kuimba kwa kufuata vyombo vya muziki na lugha ya kiarabu.
Baada ya hapo alikwenda kumtambulisha kwa wanamuziki wenziwe wa Nadi Ikhwani Safaa ambao bila kusita wakaanza kufanya naye maonyesho mbalimbali katika jamii.
Walipata mialiko mingi iliyokuwa ikitoka kwa Sultani na matajiri wengine wa kiarabu na walimtumia kwenye maonyesho mengine yakiwemo ya harusi.
Inasemekana ulifika wakati ambapo sherehe zilishindwa kufana kama Siti hakuwepo kutumbuiza kwani alikuwa moto wa kuotea mbali na jina lake lilivuma kwa haraka hadi nje ya mipaka ya nchi na bara la Afrika.
Hali hiyo ilisababisha Siti afananishwe na muimbaji wa kike aliyetamba wakati huo kutoka Misri Umm Kulthum.
Mwaka 1928 kampuni ya kurekodi muziki ya Columbia and His Master's voice yenye makazi yake Mumbai India ilisikia umaarufu wa muimbaji huyo na ikamwalika pamoja na kundi lake kwenda kurekodi kwa lugha ya Kiswahili ili kujaribu kama muziki wake utauzika.
Kampuni hiyo haikuweza kuamini jinsi muziki ule ulivyouzika kwa kasi kubwa kwani wastani wa santuri 900 ziliweza kuuzwa katika kipindi cha miaka miwili ya mwanzo na hadi kufikia 1931 santuri 72,000 zilikuwa zimeuzwa.
Kutokana na kusambaa kwa santuri hizo umaarufu wa Siti ulizidi mara dufu watu kutoka sehemu mbalimbali za dunia walifika Zanzibari kuja kumwona muimbaji huyo.
Mambo yalizidi kuwa mazuri kwa Siti hadi ikafikia hatua kampuni ya kurekodi ya Columbia kuamua kujenga studio ya kurekodi muziki Zanzibar mahususi kwa muimbaji huyo.
Hatua ya kujengewa studio hiyo iliwaumiza wengi wenye wivu na wakaanza kumtungia nyimbo za kumkejeli ili kumshusha na hasa walitumia kigezo kwamba hana uzuri wa sura, nyimbo nyingi ziliimbwa lakini huo ndio uliovuma sana

About ujugu

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments :

Post a Comment