Jahazi Modern Taarab ni bendi ya muziki wa taarab kutoka nchini Tanzania. Bendi ilianzishwa mwishoni mwa mwaka wa 2006, jijini Dar es Salaam.
Jahazi Modern Taarab, ndiyo kundi linaloongoza kwa sasa katika miondoko
ya taarab kwa nchi ya Tanzania, na ndiyo kundi pekee lenye washabiki
wengi kuliko. Kundi
limeweza kujipatia mafanikio makubwa kabisa katika medani ya muziki wa
taarab. Mzee Yusuf, ndiyo kiongozi na mmiliki wa kundi, ambaye pia ndiyo
mwanamuziki mgunduzi wa mtindo wa taarab za kisasa (yaani “modern taarab”). Mzee aliungana na dada yake Bi. Khadija Yusuf, ambaye pia ni mwimbaji
mashuhuri wa muziki wa taarab kwa nchi ya Tanzania. Wote wawili
walianza kujipatia umaarufu na heshima kubwa kimataifa wakiwa na kundi
walilokuwa zamani la muziki wa taarab la Zanzibar Stars Modern Taarab. [1]
0 comments :
Post a Comment