ABOUT US

Jahazi Modern Taarab ni bendi ya muziki wa taarab kutoka nchini Tanzania. Bendi ilianzishwa mwishoni mwa mwaka wa 2006, jijini Dar es Salaam. Jahazi Modern Taarab, ndiyo kundi linaloongoza kwa sasa katika miondoko ya taarab kwa nchi ya Tanzania, na ndiyo kundi pekee lenye washabiki wengi kuliko.
Kundi limeweza kujipatia mafanikio makubwa kabisa katika medani ya muziki wa taarab. Mzee Yusuf, ndiyo kiongozi na mmiliki wa kundi, ambaye pia ndiyo mwanamuziki mgunduzi wa mtindo wa taarab za kisasa (yaani “modern taarab”).
Mzee aliungana na dada yake Bi. Khadija Yusuf, ambaye pia ni mwimbaji mashuhuri wa muziki wa taarab kwa nchi ya Tanzania. Wote wawili walianza kujipatia umaarufu na heshima kubwa kimataifa wakiwa na kundi walilokuwa zamani la muziki wa taarab la Zanzibar Stars Modern Taarab. [1]

    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments :

Post a Comment